Tuesday, November 30, 2010

RE: SUPUUUU YA JUMAPILI TAR 28/11/2010



Raha ya Supu ya Asubuhi mara baada ya kazi nzito ya Harusi usiku wake. Hapa ni nyumbani kwa Bi mashuhuli STELLAH.
Maharusi nao hawakua nyuma kupata supu, pamoja nao alikuwepo Kishadah, Mr & Mrs Edmund, Vince, Vanessa, Evan, Eden na Dosca, kwa bahati mbaya hawakuonekana kwenye picha.
Wiki ijayo Supu wapi?

RE: MMMH NAKUMISI

Karibu jamani uwe mwanachama wa Friends Club, twakuomba jamani, mang'anyuuuuuu, Mwanamke mguu jamani

RE: USIKU WA HARUSI YA FRANK

Raha ya harusi mwishoni jamani, hii ikiwa ni kama majira ya saa 8 usiku baada ya maharusi kuondoka ukumbini, watu wanajimwaga.
Picha ya kwanza Mwenyekiti wa kamati akiwa na Mkewe wanaraha ya kumaliza Shuhuli salama.
Picha ya Pili, maharusi wa karibuni tuuu, Bw na Bi Salakana, pole Bi Salakana kwa uchovu, huwa ndo kawaida ya hawa vijana mara baada ya kumaliza Harusi,
Picha ya Tatu, Mshehereshaji Ntoli akiwa na Wapiga picha Swai na Patric huku wakiwa na Daktari wa KCMC wakimalizia vinywaji vya mwisho mwisho huku wakijadiliana mambo ya hapa na pale.
Picha ya nne, Mwenyekiti Msaidizi wa Kamati akiwa anagugumia kwa raha mara baada ya Harusi
Picha ya Tano, baadhi tu ya Vionjo vya Harusi
Picha ya Sita: Mama wa Pilika na Katibu wa Kamati Bi Stellah akiwa na swahiba wake Dosca wakisaidiana kumalizia kazi za hapa na Pale.
Poleni na Hongereni kwa kazi nzuri ya Harusi.
Nyingine Zinakuja

Tuesday, November 23, 2010

RE: MCHANGO WA HARUSI YA FRANK

Wanachama wote wa Moshi Friends Club, mnaombwa kuwakilisha michango yenu ya Harusi ya Frank Kombe kwa "Lulu au Neville" kabla ya kesho jumatano. Ni muhimu sana ili iweze kumsaidia pale alipokwama katika suala zima la Harusi yake, siku ya Jumamosi tarehe 27/11.
Mchango wako ni Muhimu sana

RE: JULIUS NA IDD

Raha ya Idd ni Pilau na Ka bia, hapa ndugu Semalli akiwa anapata ka bia kabla ya supu na Pilau ya Idd nyumbani kwa Kishadah.
Hali ya kukaa chini ni ka uchovu tu MBE

SEND OFF YA MAMA KOKU YATISHA

Mara baada ya kazi nzito iliyotupeleka Morogoro, ya kupokea Kitu cha Frank Kombe, "Mama Koku", timu nzima ilikaa na kupata picha ya pamoja, kuanzia kushoto waliosimama, Kishadah, Frank, Fortunatus, Edmund, Mrs Fortunatus & Goodluck. Aliyekaa ni Mama Koku na Kennedy.
Timu hii ilimasindikiza Frank, rafiki yao Mpendwa na Mwanachama wa Moshi friends Club katika shuhuli ya ku send off toka kwenye familia ya Kibozi, mama Koku na kumkaribisha kwenye Familia mpya ya Kombe.
Hapa panaitwa KINGSWAY HOTEL, karibu na Msamvu Morogoro.
Tunampongeza Mama Koku kwa Sherehe nzuri na iliyofana.
Baada ya kupiga picha hii, Timu nzima iliyotumwa na Friends Club ilianza safari ya kurudi Moshi.